emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WAKALA WA HUDUMA YA UNUNUZI SERIKALINI

Ununuzi Unaozingatia Thamani

Habari kwa Umma

Tangazo kwa umma

Mnamo siku ya Jumanne tarehe 18 Februari, 2025 Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe.

Paul Chacha akiwa ameambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Tabora

alifanya ziara ya kushtukiza katika ofisi ya Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini

(GPSA) Mkoa wa Tabora alitangaza kuwa amemuelekeza Katibu Tawala Mkoa wa

Tabora kumsimamisha kazi Meneja wa GPSA Mkoa wa Tabora Bw. Mayala Mburi

kupisha Uchunguzi wa tuhuma za utovu wa nidhamu.

Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA) unalaani na kukemea vitendo vya

aina yoyote vya utovu wa nidhamu katika Utumishi ambavyo ni kinyume na Sheria,

Kanuni na Taratibu za Utumishi wa Umma. Wakala unaendelea na uchunguzi na

hatimaye kuzishughulikia tuhuma hizo kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na Taratibu za

Utumishi wa Umma. Wakala umemsimamisha kazi Bw. Mayala Mburi ili kupisha

uchunguzi wa suala hilo na kumteua mara moja Bw. Stephen Muro kukaimu majukumu

ya nafasi hiyo na huduma zinaendelea.

Wakala unaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza. Wakala utaendelea

kuhakikisha unazingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za Utumishi wa Umma kwa

watumishi wake katika utoaji wa huduma zake na utachukua hatua stahiki kwa wale

wote watakaobainika kukiuka.

Wakala unawajulisha wateja wetu na Umma kwa ujumla kuendelea kuwasiliana nasi

kupitia mawasiliano yetu ya Kituo cha Huduma kwa Mteja namba 0735 005 005.

Imetolewa na

Kitengo cha Mawasiliano na Masoko

WAKALA WA HUDUMA YA UNUNUZI SERIKALINI